HATIMAYE MBEYA CITY NAYO YAREJEA LIGI KUU



KLABU ya Mbeya City imefanikiwa kurejea Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara baada ya ushindi wa mabao 5-0 dhidi ya Cosmopolitan ya Dar es Salaam jioni ya leo Uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya.
Mabao ya Mbeya City leo yamefungwa na Riffat Msuya dakika ya 16 na 28, Eliud Ambokile dakika ya 40, Faraji Kilaza Mazoea dakika ya 59 na David Mwasa dakika ya 70.
Kwa ushindi huo,Mbeya City inafikisha pointi 65 na inakamilisha idadi ya timu mbili za kupanda baada ya Mtibwa Sugar yenye pointi 68 kufuatia timu zote kucheza mechi 29.
Mbeya City inarejea Ligi Kuu baada ya misimu mitatu tangu ishuke daraja msimu wa 2021-2022 kufuatia kupanda kwa mara ya kwanza msimu wa 2013-2014.



Sultan Uwezo

In our hands you will find out Songs and Videos of Various Artists without forgetting News from Newspapers. Here you will also find Employment's Information from the Government and the Private Sectors.

Post a Comment

Previous Post Next Post