NITAKUUA MWENYEWE - 92
sultanuwezotz.blogspot.com
Huku nyuma Jackline aliitoa bastola yake na kuivisha kiwambo tayari kwa kuzuia mlio kusikika kisha akairejesha kwenye koti lake. Mara alitokea mwenyekiti akiwa kaongozana na mke wake, alipokutana na sura ile ya Jackline ni kama alihisi kitu.
"Karibu binti."
"Asante."
Aliitikia Jackline.
"Ndiyo sijui nikusaidie nini binti."
Mwenyekiti alimuuliza Jackline.
"Sidhani kama unaweza kunisaidia kitu chochote mwenyekiti."
Jackline alimjibu huku akikaa vizuri kitini.
"Hudhani kama naweza kukusaidia?"
"Ndiyo huwezi kunisaidia chochote."
"Heee !! Sasa kama sina cha kukusaidia umefuata nini kwangu muda huu?"
"Nimekufuata wewe, unakumbuka jana uliniambia una tatizo gani?"
Jackline alimjibu huku akiinuka pale alipokuwa kakaa.
"Wewe binti hebu kuwa na adabu unapoongea na kiongozi mkubwa wa eneo hili, sawa !!"
Mwenyekiti aliongea kwa hasira kidogo huku akiwa kamtolea macho Jackline.
"Niwe na adabu ninapoongea na kiongozi mkubwa wa eneo, nani huyo wewe au mwingine?"
Hapo Jackline alimsogelea mwenyekiti na kumkamata kidevu huku akimuuliza maswali kwa sura iliyojaa hasira.
Kitendo kile kilimkwaza mke wa mwenyekiti aliinuka pale alipokuwa kakaa na kumfuata Jackline bila kuuliza aliinua mkono ili ampige lakini alikutana na teke ambalo lilimpeleka mpaka kwenye meza na kujipigiza huko.
"Mume wanguuu.....niokoee....!!"
Alipiga kelele hizo huku akibubujikwa na damu kichwani. Mume wake alitaka kumfuata mke wake ili atoe msaada lakini alishangaa kukutana na mdomo wa bastola.
"Sasa unaweza kupata majibu ya maswali yako kwanini niko ndani ya nyumba yako, ili kuokoa uhai wako na wa mke wako ongea mwenyewe ulichokifanya nyumbani kwa mzee Jerome."
"Binti mbona sijafanya lolote mimi huko?"
Alijitetea mwenyekiti.
"Ohh vizuri sana kumbe siyo wewe....!!"
Jackline aliongea na kumtandika risasi ya kidole cha mguuni.
"Mwenyekiti unaweza kuongea sasa bila uoga wowote."
Kabla hajajibu chochote mwenyekiti alichomwa kisu cha kwenye paja ambacho kilimfanya kupiga ukelele wa maumivu huku mke wake naye alikuwa akiendelea kuvuja damu bila msaada wowote.
"Vipi mwenyekiti bado huna majibu ya swali langu?"
Alimuuliza huku akiwa kamsogelea karibu zaidi.
"Nitaongea ukweli wote ila naomba usiniue binti yangu."
"Unanichelewesha mzee ongea haraka."
"Usiku ule nilifuatwa na mwanadada aitwaye Nafiwe akiwa kaongozana na watu wengine wawili wa kiume ambao sikujua majina yao lakini walikuwa wageni machoni pangu na kisha kunishinikiza nije pale niwazubaishe kisha niondoke, lakini sikujua nini maana yake na mara baada ya mimi kufanya vile na wale vijana tulirudi majumbani na baada ya kama dakika thelathini hivi alirejea Nafiwe peke yake akiwa na furaha kubwa hakusema kitu zaidi ya kunikabidhi bahasha ya kaki iliyokuwa na hela ndani yake."
"Ni hivyo tu?"
Jackline alimuuliza tena.
"Ni hivyo binti yangu lakini anapotoka alisema nisiwe na wasiwasi juu ya usalama wangu kwani wao wanaelekea mafichoni Brazil kwani walichokuwa wanakihitaji wamekipata."
"Walichokuwa wanakihitaji wamekipata?"
"Ndiyo."
"Kitu gani hicho?"
"Hapo ndiyo sifahamu chochote."
Majibu ya mwenyekiti yalipiga kengele ya hatari kwa Jackline akiamini kuwa kwa vyovyote vile wamewachukua Jasmine na Titiana kwa ajili ya kwenda kuwatoa viungo vyao vya mwili kama ilivyokuwa ahadi ya Santana ili wakaviuze kwa Wahindi huko India hivyo hakuona sababu ya kuchelewa kubaki alimchapa risasi mbili za utosini mwenyekiti huku mke wake akimshindilia kisu cha tumboni kisha kutoka zake. Alitembea haraka sana kuelekea nyumbani kwa mzee Jerome tayari kwa safari. Lakini alipofika nyumbani kwa mzee Jerome Whistle aliwakuta Jessica na Roberto nao wakiwa tayari na mizigo yao kwenye gari alilopakia yeye.
"Enhh mbona mko hapa?"
Jackline aliwauliza baada ya kuwakuta wakiwa wameegemea gari.
"Tulikuwa tunakungojea wewe hatuko tayari kutengana na wewe katika hili hivyo na sisi tunaambatana pamoja huko uendako."
Roberto alimweleza Jackline kile walilokuwa wamejadiliana baada ya yeye kuondoka pale hospitali.
"Vizuri lakini mimi siko tayari kuongozana na ninyi popote naogopa kuwaharibia mikakati yenu bwana, nilianza tukakutana njiani naomba tuachane njiani safari nitaimaliza mwenyewe."
Jackline aliongea na kuingia kwenye gari lakini kabla hajaondoka wakina Roberto waliingia garini.
" He vipi ninyi naomba mshuke mnanichelewesha jamani!!!"
" Fanya chochote juu yetu lakini hatuko tayari kufanya kosa jingine ambalo litasababisha tukupoteze."
Jessica alimjibu Jackline majibu ambayo yalimchosha na kupelekea kupiga mikono yake kwenye usukani kisha akageuka kuwaangalia kwa macho ya hasira kisha alijifunga mkanda na kuwasha gari safari ikaanza. Walianzia kwenye makazi ya Madam Nafiwe kwanza ambako baada ya kufika kila mmoja alikamata silaha mkononi na kugonga geti la nyumba hiyo humo kila mmoja alielekea upande wake lakini mwishoni walikutana wakiwa hawana walichokiona kwenye jengo hilo hivyo waliingia kwenye gari na kuelekea kwenye jengo jingine la Nafiwe.
"Tumefika kwenye jengo hili ambalo Nafiwe hulitumia kama ofisi za kampuni yake hivyo tuweni makini wanaweza kubadili matumizi kwa muda."
Jackline aliwatahadharisha wakiwa wanashuka kwenye gari.
"Tufanye kipi dada Jackline?"
Jessica aliuliza swali.
"Tutaingia kwa pamoja silaha zikiwa mifukoni kisha upepo ukibadilika tu ni kuzichomoa na kucheza nao."
"Bila shaka."
Roberto alijibu kisha wakashuka kwenye gari na kuliendea geti ambalo halikuwa mbali na pale walipokuwa, walifika na kugonga. Mlinzi alifungua na kuwaruhusu waingie ndani walitazamana na kuingia Jessica akiwa mbele Roberto akifuata na Jackline akawa wa mwisho na baada ya kumpita tu mlinzi Jackline aligeuka na kumpiga teke la kidevu ambalo lilimpeleka chini mlinzi na bila kuchelewa alimfuata na kumkita kisu cha kifuani wakina Jessica walipogeuka na kuushuhudia mchezo ilibidi wafichame kwa lengo la kumlinda ili alitokea mjinga yeyote wacheze naye.
"Niambie Nafiwe yuko wapi na watu wake?"
Jackline alimuuliza mlinzi huyo huku akikizungusha kile kisu alipomchoma.
"Aghh.. Si..si...ju..ju.. Mamaaaa nitaongea usinifanye hivyo wewe mwanaizaya."
"Ongea haraka kabla sijaanza kuondoa vidole vyako."
"Wam...wam....eondoka muda si mrefu kue...kuelekea bandarini wanataka kuiwahi Meli ya usiku."
"Wameondoka wangapi?"
"Waliku...wali...wa...wakuwa wote na wa...wal...."
Hakumaliza sentensi yake alikata kauli.
Aliinuka na kuwapa ishara wenzake ya kuondoka mle ndani.
"Tunaelekea bandarini muda huu inasemekana wako huko wanajiandaa kusafiri na Meli ya usiku ila haijulikani ya saa ngapi, muda huu ni saa moja hebu tuwahi huko."
Aliwaelekeza alichoambiwa na mlinzi kisha walitoka na kuelekea walikokuwa wamepaki gari lakini walipolikaribia gari Jackline alilishtukia baada ya kuona ni kama kuna kivuli cha mtu hivyo aliwazuia wenzake wasilisogelee.
" Jessica msilisogelee hilo gari ni kama kuna mtu kwa nyuma."
"Kuna mtu?"
Roberto aliuliza huku akiliangalia gari hilo pale lilipokuwa kama kuna mtu kweli.
NINI KITAENDELEA?
TUKUTANE KATIKA SEHEMU INAYOFUATA YA HADITHI HII YA KUSISIMUA.
YA KUTAFUTIA USINGIZI HIYO.
#SULTANUWEZO