NITAKUUA MWENYEWE - 68 (Mtunzi: Sultan Uwezo)

 


NITAKUUA MWENYEWE - 68

sultanuwezotz.blogspot.com 


"Jackline mwanangu naomba niongee kitu ili baada ya hapo chukua uamuzi."

Mke wa mzee Jonathan aliongea, muda huo wote walikuwa wamefungwa kwenye mizizi ya mti ulio ndani ya kimto kilichokatisha ndani ya pango hilo na kuifanya sehemu ya miili yao kuwa majini na kuanzia kifuani kuja kichwani kuwa nje ya maji. Na wakati huu mzee Kaaya ya mke wake walishatolewa ndani ya maji wakiwa hawajitambui kabisa japo ilikuwa kwa mzee Jonathan ambaye naye alikuwa amekata kauli lakini hawakumtoa ndani ya maji,aliendelea kusalia humo.

"Unasema nini wewe Shetani? Au unafikiri sijui ambacho ulikifanya na mumeo kwa wazazi wangu, wewe si ndiye ulimshawishi mume wako kuwaendea kwa mganga ili muweze kumiliki Mali zetu? Kwa mfano mngechukua tu mali na kuwaacha wazazi wangu tusingefika huku."

Jackline alimkatisha mama yake mlezi huku akiwa kajifunga jaketi lake kiunoni na kuuacha mwili wake ukisitiriwa na kibana maziwa tu na kuliacha tumbo lake likiwa wazi nafikiri ni kutokana na shughuli pevu waliyokuwa nayo mle pangoni. Na muda huu wengine kama Jasmine, Jessica, Roberto na Titiana wakiwa wanamuandaa swala ambaye alikuwa kanaswa na mtego wa Titiana ambao alikuwa kautega nje ya pango.

"Mwanangu ni kweli kabisa na yote hii ilikuwa ni kutokana na uroho wa mali ambazo tuliamini zingekuwa mikononi mwetu baada ya kukumaliza wewe lakini hali ya hewa imebadilika na sasa wewe umegeuka kuwa hakimu wa haya, tunaomba huruma yako mwanangu usiibebe roho ya kikatili ambayo hukuwahi kuwa nayo.. "

Aliongea huku akilia mama huyo.

"Kaa kimya mwanaharamu wewe, mchawi usiye na tunguli wala ofisi elewa kuwa Jackline umuonaye hapa si yule uliyemfahamu kipindi iko huyu ni mwingine kabisa ambaye hujawahi kumuona wala kumsoma kwenye kitabu chochote kile, ninachokuomba ni kufunga hili domo lako lililosheheni kila aina ya unyang'anyi."

Jackline aliongea hayo huku akimgusa mdomo kwa bastola yake.

" Oho! oho! oho!..... "

Mzee Jonathan alizinduka na kuanza kukohoa.

" Roberto njoo umfungue Rastaman naona tayari karudi duniani baada ya kuona alikokuwa ni afadhali ya duniani."

Jackline alimwambia Roberto baada ya kumsikia mzee Jonathan akikohoa.

"Naja kamanda wangu mwenyewe."

Roberto alijibu akikata kipande cha nyama na kukitupia mdomoni.

"Mwanangu naomba usiniite hivyo hii yote ni katika kujaribu kuukwepa mkono wa sheria yote kwa yote ninaomba uukunjue moyo wako uliojikunjakunja kutokana na niliyokufanyia, kisha tuliweke sawa hili niko tayari kwa lolote."

"Unaongea nini wewe mwanaharamu usiye na haya wala aibu, nisikilize kwa makini wewe mzee mali zetu utazitoa kwa hiari au kwa lazima. Unanielewa?"

Jackline alimuuliza mzee Jonathan ambaye muda huo alikuwa taabani kwa mateso.

"Mzee acha kusinzia unamsikia Malkia wa Haki anayokwambia?"

Roberto alimuuliza akiwa anamfungua pingu za miguuni.

"Nimemsikia kijana wangu tena vizuri tu."

Mzee Jonathan alimjibu Roberto.

"Kwa hiyo unasemaje katika hili au unasubiri mpaka tukufanyie umafia?"

Jackline alimuuliza swali kutokana na majibu yake kwa Roberto.

"Niko tayari kurudisha mali zako binti kikubwa tu uniahidi kuwa utaniacha huru na mke wangu tuanze maisha mapya."

Mzee Jonathan alimjibu akiwa anajiinua ili apige magoti kuomba msamaha, lakini ikawa tofauti kwani Roberto alijua anataka kuinuka ili aanze vurugu hivyo alichokifanya ni kumtwanga bonge la teke lililomkuta kifuani na kumpeleka ndani ya kijito cha maji na kujigonga gonga huko na kusababisha kichwa chake kupasuka sehemu ya paji lake na kupelekea damu nyingi kumtoka.

"Jamani mbona hivi? Basi kama lengo ni kuniua naombeni mfanye hivyo mapema kuliko haya mnayoendelea kunifanyia."

Alipaza sauti akiwa majini akijivuta kutoka nje.

"Mzee nakuonea huruma sana ni bora ufanye fasta tumalize mchezo wetu."

Roberto alimwambia akiwa anampa sapoti ya kumtoa majini kwa staili ya tanganyika jeki.

"Jackline tufanye fasta hili eneo tuondoke maana si salama tena kwetu si mnawakumbuka wale wawindaji wa jana mnafikiri watakaa nalo hili pamoja na mkwara tuliowachimba?"

Jasmine alikuja akila nyama na kuwataka zoezi liende haraka ili waondoke zao hapo.

"Nakumbuka vizuri sana ndugu yangu si hawa washenzi wanajitia ugumu wakati tayari washaanza kuwa mkate mbele ya Chai."

Jackline alimjibu Jasmine.

"Eti mzee kuna ugumu unaouleta mpaka muda huu? Mimi nilikuwa kimya kwa sababu ya njaa na kwa sasa niko fiti kukipokea kijiti hiki hivyo basi unaweza tu kurahisisha mambo mwenyewe ili tusifike huko na haya yote yanatokea kutokana jeuri yako mzee sisi hatuna roho mbaya kiasi hicho ila wewe ndiyo unafanya tuwe hivyo."

Jasmine alimsogelea mzee Jonathan na kuanza kumtisha kiaina.

" Mbona mimi sina tatizo kabisa hata hapo awali nimeongea jamani?"

Mzee Jonathan alitokwa na maneno.

" Huna tatizo ee basi tuuanze mchezo wetu pasipo sababisha majanga zaidi mzee manywele."

Jasmine aliona ubebe msala baada ya kuona wakina Jackline kama vile wamevurugwa.

Wakati Jasmine akiuanza mchezo na mzee Jonathan kwa kumfanya kukubali kumkabidhi Jackline kila kilicho chake simu ya Jackline iliita na hivyo kuichukua na kuangalia mpigaji hakuwa mwingine bali Santana.

"Nakusikiliza Mwanaizaya usiye na haya."

Jackline alianza baada ya kupokea simu ya Santana.

"Nisikilize wewe mrembo, na waambie na hao Warembo wenzako kuwa ninyi bado sana kwenye hili gemu. Na kuhusu lile deo lenu mlilomrekodi mzee wa Robinson wala halitustui hata chembe kwani hao muda wao wa kuishi umefika ukingoni na Robinson anachokiangalia ni maisha yake kwani kwa sasa hana mpango wa kurudi Tanzania sijui Afrika hivyo msijidanganye na vimichezo vyenu visivyo na kichwa wala miguu, umenielewa? "

Santana alihitimisha kwa kuuliza swali.

" Umeshamaliza ambayo ulipanga kuyaongea kwetu?"

Jackline naye alimtupia swali.

" Pigia mstari kama bado au la."

Amjibu Santana.

" Kata simu basi sisi huku tuna majukumu ya kifamilia na si kitu kingine wewe Mbwamwitu."

Jackline aliona ampakie Santana.

"Na muda si mrefu mtapokea matokeo ya gemu linaloendelea kuchezwa hapo hapo Namibia."

"Unasemaje?"

Jackline aliuliza kwa hamaki swali ambalo hata hivyo halikupata jibu kutokana na simu kukatwa na Santana, kitendo kilichoshuhudiwa na Jasmine pamoja Roberto baada ya kumuona Jackline ameishiwa pozi baada ya kukatwa simu.

"Anasemaje huyo Santana?"

Jasmine alimuuliza Jackline.

"Kuna tatizo tayari Namibia kwani inavyoonekana tayari Santana na watu wake wako Namibia na hofu ni kwa familia ya mzee Jerome, ya Daktari Abbas Mukesh na ya Daktari Hans Murray."

Jackline aliongea kwa yale aliyoyaamini kumhusu Santana.

"Tunafanyaje hapo?"

Roberto alimuuliza Jackline na Jasmine.

"Hebu ngoja kwanza."

Jasmine aliongea hivyo huku akiipekua simu na baada ya kuikuta namba aliyokuwa akiitafuta na aliipiga.

"Halo baba shikamoo!"

"Marahaba mwanangu Jasmine wazima huko?"

Mzee Jerome alimuuliza Jasmine.

"Sisi tu wazima kabisa vipi kuhusu ninyi?"

Jasmine alimjibu na kumuuliza swali.

"Sisi ni wazima kabisa na biashara zetu zinakimbia kama upepo sijui kwanini mlichelewa kuja kwenye familia yetu hakika ninyi ni Malaika wetu."

Mzee Jerome aliongea kwa furaha.

"Hongereni sana lakini kuna janga linawavizia na ndiyo maana nimekupigia mzee wangu."

"Janga gani Jasmine mbona unataka kuniweka kiroho juu mzee wako?"

Mzee Jerome alichanganyikiwa baada ya kusikia hivyo.

"Mzee ni hivi hapo Namibia kuna watu wamekuja kututafuta baada ya yule mwanzo kuminywa mdomo wakaona hakuna jingine zaidi ya kuwatuma wengine hivyo hofu yetu ni kama wakitukosa."

"Hofu ya nini mwanangu huoni kama wakiwakosa wataondoka zao."

"Si hivyo baba, tunahisi wanaweza kuwakamata ninyi na ikiwezekana kuwafanya kitu mbaya."

"Inawezekana eti eee??"

"Ndiyo hivyo baba hivyo kuanzia sasa chukueni hatua rafiki ya kujilinda."

"Nashukuru kwa ushauri mwanangu kwa hilo ondoa shaka si unatufahamu wavuvi tulivyo zaidi ngoja niwajulishe wakuu wa hospitali zile za Makambi na King's pia wadogo zenu."

Mzee Jerome hakuonyesha wasiwasi wowote japo alipata mshtuko mwanzoni. Hivyo Jasmine hakuona sababu ya kuendelea kuongea na mzee Jerome alimkatia simu.

" Vipi anasemaje mzee wetu? Maana kwa ubishi wake sijui."

Jackline alimuuliza japo alisikia kila kitu kutoka kwa Jasmine. 

"Eti tumuani kwani yeye hawaogopi ila atafanya maandalizi na vile vile kasema ngoja awasiliane na Madaktari pamoja na wakina Victor juu ya hili."

"Shauri yake aendelee kupingana na anachoambiwa hivi anaijua akili ya Santana?"

Jackline alimjibu Jasmine.

Kisha alimfuata mzee Kaaya ambaye akili ilikuwa iko sawa baada ya kurejewa na akili yake sasa na kumtupia swali. 

"Hivi mzee wangu hujawahi kusikia lolote kutoka kwa mwanao?" 

"Wacha nijilaumu mwenyewe kwa haya yanayotokea kwangu na familia yangu." 

Mzee Kaaya alimjibu Jackline. 

"Kivipi mzee Kaaya?" 

"Utu wangu unanimaliza mwenyewe, hivi Jackline wewe ni wa kutufanyia haya kweli?

Tule nyama basi si tayari umetuivisha."

Mzee Kaaya aliongea kwa hisia kali na kuanza kulia kwa kwikwi. 

"Labda nikuulize swali jepesi tu mwanangu Jackline." 

Mzee Kaaya aliinua kichwa na kumuomba amuulize swali. 

"Uliza tu mzee kama ukiweza." 

Jackline alimjibu mzee Kaaya. 

"Hivi huyo mwanangu mnayemwita msaliti mara jambazi ambaye mnasema lazima mmuue usingeondoka naye kwenda huko mlikokuwa angekuwa hivyo alivyo?" 

"Mzee Kaaya kumbe bado unajeuri kama mwanao eee?" 

Mzee alijikuta alikutana na kofi la machoni baada ya kumuuliza swali Jackline ambalo bila shaka lilimwingia na kujikuta akifanya kitendo hicho ambacho kilipelekea mzee Kaaya kwenda chini. 

"Sawa nifanye chochote Jackline lakini kumbuka kuwa mimi ni mtuhumiwa nisiye na hatia mwenyewe mnamfahamu fika na hata kama nitakufa leo hii lakini ukweli utabakia pale pale." 

Aliongea maneno hayo ambayo yalimwinua Jackline na kutoka mpaka nje ya pango lile na kwenda kukaa karibu zaidi na magari huko alianza kulia kwa sauti ya chini kwani alichoambiwa na mzee Kaaya ilikuwa kweli tupu japo yeye alijua alichokuwa anakihitaji kutokana na kuwashikilia wazee hao.


NI NINI KITATOKEA HUKO PORINI NA NAMIBIA?


TUKUTANE KATIKA SEHEMU INAYOFUATA.


        #SULTANUWEZO

Sultan Uwezo

In our hands you will find out Songs and Videos of Various Artists without forgetting News from Newspapers. Here you will also find Employment's Information from the Government and the Private Sectors.

Post a Comment

Previous Post Next Post